Madereva Bajaji Wafunga Barabara Morogoro....Jeshi la Polisi Lawatuliza.

Baadhi ya madereva wa bajaji mjini Morogoro wamelazimika kufunga barabara kufuatia kamatakamata ya polisi iliyofanyika katika mji huo mapema leo.
Madereva hao wamesema wamefikia hatua hiyo baada ya askari polisi na askari wa akiba kuzingira katika maeneo mbalimbali ya katikati ya mji pamoja na kituo cha daladala na kuzikamata bajaji zao.
Hatua hiyo ikakilazimu kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Morogoro kikiongozwa na Kamanda Michael Daleli kuingilia kati na kufanikiwa kutuliza ghasia pamoja na kuondoa msongamano uliosababisha shughuli mbalimbali kusimama.
"Barabara iligeuzwa kuwa kituo cha maegesho ya bodaboda na bajaji, sasa tunazifungua na nyinyi ni mashahidi hata misafara iliyokuwa inapita eneo hili ilikuwa inazunguka mbali sana kuelekea pale Ikulu ndogo", amesema Kamanda Daleli.
Naye Mratibu wa Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini TARURA, Mhandisi Godwin Mpinzile amesema kuwa madereva hao walipewa sehemu za kwenda kuegesha magari yao lakini wamekuwa wakikaidi na ndiyo maana zoezi hilo limefanyika.
Rais Magufuli Amjulia Hali Mkurugenzi Mkuu Mstaafu wa Idara ya Usalama wa Taifa Apson Mwang’onda.

Waziri Wa Kilimo Japhet Hasunga Afanya Mazungumzo Na Ujumbe Wa Wakurugenzi 6 Wa Mashav Nchini Israel

Na Mathias Canal, Jerusalem-Israel
Waziri wa Kilimo wa Tanzania Mhe Japhet Hasunga (Mb) leo tarehe 5 Septemba 2019 amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Wakurugenzi 6 wa Mashav wa Wizara ya Mambo ya nje ya Israel.
Katika mkutano huo wa kazi uliofanyika katika Ofisi za wizara ya Mambo ya nje ya Israel iliyopo mtaa namba 9 Yitzhak Rabin Jijini Jerusalem nchini Israel, Waziri wa Kilimo amewasilisha mambo mbalimbali kuhusu sekta ya kilimo ikiwemo ufuatiliaji wa utekelezaji wake.
Mhe Hasunga ameishukuru serikali ya Israel kwa kukubali ombi la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli la kuongeza idadi ya wanafunzi wanaoshiriki mafunzo ya Kilimo ya Agro Studies katika kipindi cha mwaka mmoja kutoka 45 ambapo imefikia idadi ya wanafunzi 100.
Katika kikao hicho Waziri Hasunga amewakumbusha Mabalozi hao sita kuhusu ombi la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli la kuongezwa idadi ya wananfunzi kufikia idadi ya wanafunzi 300.
Mhe Hasunga amesema kuwa Balozi huyo amepongeza kwa dhati na kuunga mkono juhudi za serikali ya Tanzania inayoongozwa na Mhe Dkt John Pombe Magufuli kwani ni serikali ya vitendo na uwajibikaji hivyo wapo tayari kuhakikisha kuwa ushirikiano unaboreshwa baina ya nchi hizo mbili.
Kikao hicho pia kimejadili kwa kina namna ya kuboresha zaidi mahusiano baina ya nchi ya Tanzania na Israel hususani katika kuimarisha ushirikiano kwenye nyanja za utafiti, uongezaji thamani wa mazao, na namna ya kuongeza ukubwa wa mashamba na kilimo tija.
Pia, Mhe Hasunga amewasilisha ombi la kupata kampuni mbalimbali za nchini Israel ili kuzuru Tanzania na kuwekeza kwenye kilimo cha umwagiliaji.
“Tukipata kampuni za kuisaidia Tanzania kwenye maswala ya kilimo cha umwagiliaji tutakuwa na fursa ya kubadili kilimo chetu kutoka kwenye kilimo cha kutegemea mvua na hatimaye kuingia katika kilimo cha umwagiliaji” Alisisitiza Mhe Hasunga na kuongeza kuwa
Serikali ya Israel imekubali kufikiria kuongeza idadi ya vijana kutoka Tanzania wanaozuru Israel kwa ajili ya kujifunza ambapo pia wataongeza uwezekano wa wataalamu mbalimbali wakiwemo maafisa ugani nchini Tanzania kuzuru Israel kwa ajili ya kujengewa uwezo katika utendaji.
Kwa upande wake Naibu Mkurugenzi wa Taasisi ya Maendeleo ya Ushirikiano wa mambo ya nje nchini Israel Ndg Yuval Fuchs amesema kuwa serikali ya Israel imeridhia maombi ya Waziri wa Kilimo wa Tanzania Mhe Japhet Hasunga na kusema kuwa Israel ipo tayari kushirikiana na Tanzania ili kuboresha sekta ya kilimo kutoka kwenye kilimo cha kujikimu kuwa kilimo cha kibiashara
Vilevile amesema kuwa atazishawishi kampuni mbalimbali kuwekeza nchini Tanzania kwa ushirikiano mzuri na serikali kwani Tanzania kuna ardhi nzuri yenye rutuba kwa ajili ya kilimo.
Kadhalika amempongeza Waziri Hasunga kwa kutembelea nchini Israel kwa ajili ya ziara ya kikazi ambapo amesema kuwa kumekuwa na kikao muhimu kilichojadili namna ya kuboresha kilimo nchini Tanzania.
Kadhalika, Balozi wa Tanzania nchini Israel Balozi Job Daud Masima amesema kuwa kikao cha Waziri wa Kilimo ni muendelezo wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo nchini Israel ambapo ameongeza kuwa kikao hicho kimetoa taswira ya kutafakari kwa pamoja kuona namna mafunzo hayo yanavyowasaidia vijana wa kitanzania.
'Mrithi' wa Tundu Lissu aapishwa rasmi, mahakama kutoa uamuzi Septemba 9

Miraji Mtaturu, kutoka Chama Cha Mapinduzi, CCM, ameapishwa rasmi hii leo kuwa mbunge wa Singida Mashariki.
Mtaturu anachukua kiti hicho cha ubunge ambaho awali kilishikiliwa na Tundu Lissu aliyevuliwa ubunge wake na Spika Job Ndugai mnamo Juni 28 mwaka huu.
Tundu Lissu amekuwa nchini Ubelgiji akipokea matibabu baada ya kushambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana mchana wa Septemba 7 mwaka 2017.
Lakini wakati akiwa huko Spika Ndugai alimvua ubunge kwa madai kwamba hakuwa ametoa taarifa rasmi ya alipo, na pia hakuwa amejaza fomu za mali na madeni ya viongozi wa umma.
Mtaturu alitangazwa mbunge mteule wa jimbo hilo kwa kupita bila ya kupingwa katika hatua za awali za matayarisho ya uchaguzi mdogo baada ya wagombea 12 wa vyama vya upinzani kutorejesha fomu.
Uchaguzi huo mdogo ulikuwa ufanyike Julai 31, lakini haukufanyika tena kutokana na wapinzani kutokurejesha fomu zao.
Hata hivyo, kuna kesi mahakamani ambayo inaweza kuathiri kiapo cha Mtaturu hii leo pale ambapo maamuzi yake yatakapotolewa wiki ijayo.
Kesi hiyo imepelekwa mahakamani na Lissu akipinga kuvuliwa ubunge wake.
Yalijoriri mahakamani jana
Hapo jana mawakili wa Lissu walitarajia kuzuia kuapishwa kwa Mtaturu hii leo hadi pale kesi hiyo itakaposikizwa na kuamuliwa.
Hata hivyo, Jaji Sirillius Matupa wa Mahakama Kuu ya Tanzania alilikataa ombi hilo la mawakili wa Lissu akisema katika kesi za ubunge hata kama mtu ameapishwa anaweza kuvuliwa ubunge pamoja na kiapo chake.
Kesi hiyo hapo jana iliunguuma mpaka saa tatu kasoro robo usiku ambapo Jaji alitangaza maamuzi yake juu ya ombi la kiapo cha Mtaturu.
Jaji Matupa amesema kuhusu maombi rasmi ya Lissu kupinga kuondolewa katika ubunge yatatolewa Septemba 9, 2019.

Lissu amefungua maombi chini ya hati ya dharura, kupitia kwa kaka yake Alute Mughwai, ambaye amempa mamlaka ya kisheria kufanya hivyo, akitaka kurudishiwa ubunge wake.
Lissu anapinga vikali kuvuliwa wadhifa wake akidai kuwa amefutwa ubunge huku ikifahamika wazi kuwa amekuwa nje kwa matibabu tangu tarehe 7 mwezi Septemba mwaka 2017, baada ya kushambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana.
Mwanasiasa huyo hapo awali aliiambia BBC kuwa alitarajia hatua zilizochukuliwa na Spika dhidi yake kwa sababu alishasema kwa hiyo ilipotokea mwezi wa sita wala haikuwa ajabu.
''Mtu ambaye alishakuwa na nia ya kunifuta ubunge nisingeweza kumzuia, vinginevyo labda ningesema niachane na habari ya matibabu nirudi Tanzania''.
0 Reviews:
Post Your Review